Wednesday, August 10, 2011

Samsasali blogspot. Huyu jamaa ni noumer!

Kibogoyo Wake Mtori, Supu ataambulia Mchuzi.

Ni matumaini yangu ya kuwa wote tu wazima baada ya Long Weekend leo wengi tumerejea katika shughuli zetu za kile siku. Poleni na pilika pilika za Mafuta hapa mjini Dar-es-Salaam hali imekuwa tata, leo nimesikia watu wakiwalaumu EWURA kusababisha matatizo kwani wao walikuwa wananunua bei hiyo wanayotaka kimbelembele cha EWURA kujifanya inawajali wananchi kumbe ndo imewakera wananchi hahaha Tanzania ni Zaidi ya uijuavyo.

Ninakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya Friends On Friday ya tarehe 5 August, 2011 haikuwa ya Kitoto Sifa na Utukufu tunamrudishia Mungu.

Katika utafiti wangu nimegundua watu wengi sana maarufu ama mashuhuri, umaarufu wao na umashuhuri wao uliwajia kama ajali, haikuwa katika moja wapo ya plan za maisha kufika pale walipofika, ndio maana wengi wao huwa hawadumu katika kile kilichowaweka juu, utakuta mtu ame struggle kufika sehemu fulani katika maisha ila akifika hapo juu anaanza kufanya mambo yanayommaliza yeye mwenyewe.

Shauku yangu nikiona watanzania hasa vijana kila Mtu aki simama kutimiza ndoto ya maisha yake, na nini unafanya kutimiza ndoto za wengine pia, mimi kama leo nimenyanyuliwa ninafanyaje kuwainua wengine. Wabongo wengi sisi ni vibogoyo inapofika swala la kutimiza ndoto zetu. Wengi tunapenda mambo mepesi mepesi hatupendi Big Stuff.

Kuna msemo ambao ni maarifu sana ulioongelewa naAliyekuwa Kiongozi wa Marekani Aleanor Roosevelt, aliwahi sema "Great Mind discuss about Ideas, Average Minds discuss Events and Small Minds Discuss People"

(Mengi zaidi yapo katika blogu yake... Jamaa ni creative nimependa sana.. We kamcheki halafu urudi uniambie umeonaje?)

1 comment: