Sunday, October 9, 2011

Muziki wa Injili isiwe Biashara - Ency Mwalukasa

"NYIMBO na muziki wa Injili ni wito na si biashara kama watu wanavyofikiria.

"Waimbaji wa nyimbo za injili tuimbe nyimbo kwa wito na si kwa ajili ya kutaka kutafuta pesa au kugeuza wito huo kama ajira.

"Waimbaji wengi siku hizi hawaimbi kwa kuwa wanapenda au wanataka kumtukuza Mungu, ila wanafanya hivyo kwa ajili ya kutimiza maslahi yao binafsi."

Hivyo ndivyo anavyoanza simulizi lake, msanii Ency Mwalukasa, mama wa familia ya watoto watatu ambaye pia ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili nchini ambaye pia ni miongoni mwa wasanii wanaotamba kwa sanaa hiyo.Msanii huyu ambaye ana asili ya Mkoa wa Mbeya, kwa sasa anaishi jijini Dar es Salaam akiwa na na familia yake.Anasema ameamua kujishughulisha na uimbaji ambao unaambatana na kulisambaza neno la Mungu kwa njia ya sanaa ya uimbaji.

Mwanadada huyo anaeleza kuwa alianza kuzama katika usanii tangu akiwa Shule ya Msingi Sisimba iliyoko Mbeya na baadae katika Shule ya Sekondari Mbeya alikosoma na kuhitimu kidato cha nne.Anasimulia kuwa baada ya elimu ya kdato cha nne alifaulu vizuri na kuwa kati ya wale waliochaguliwa kwa ajili ya kujiunga na kidato cha tano ambako alipangiwa Shule ya Sekondari Jangwani ambako alisoma hadi kidato cha sita.Akiwa Jangwani, msanii huyo anaeleza kuwa nako alifanya vizuri katika mtihani wake wa kidato cha sita na baadaye kujiunga na chuo cha kompyuta kilichopo nchini Zambia kiitwacho Legacy Computer Institute ambako alisoma kwa muda wa mwaka mmoja na kuhitimu masomo hayo.

Baadaye, mwaka 1992-1994, Mwalukasa alifanya kazi katika mashirika mbalimbali, ingawa ilikuwa kwa kipindi cha mwaka mmoja, akiwa katika shirika la kidini na African Evangelistic Enterprise.Shirika hilo, Mwalukasa anasema lilikuwa likijihusisha na masuala ya huduma za kiroho na usambazaji wa neno la Mungu katika sehemu mbalimbali za Afrika.Baada ya kutoka katika shirika hilo, alijiunga na shirika jingine liitwalo Mission Aviation Fellowship(MAF) kwa muda wa miaka miwili na baada ya hapo alijiunga na El Akiwa katika shirika hilo la MAF, mwanamama huyo anasema kuwa akishughulika na shughuli za utoaji wa huduma ya neno la Mungu katika sehemu mbalimbali nchini Tanzania.

Mwanamama huyo anasema kuwa baada ya kufanya kazi katika mashirika yote hayo, ndipo akaamua kufundisha dini katika shule mbalimbali . Huko alifundisha dini na maadili mema, wakati huo akiwa chini ya shirika la Scripture Union ambako alifanya kazi kwa muda wa miaka mitano.

Kwanini aliamua kufanya kazi katika mashirika ya dini?

Anajibu kuwa ni kutokana na jinsi alivyokuwa akiipenda dini na hadi leo anaamini kuwa yeye ni kati ya watu wachache ambao wameteuliwa kufanya kazi ya kumtukuza Mungu."Hata siku moja sijutii kazi nayo ninayoifanya ambayo ni ya wito, kwani najisikia furaha na mwenye amani kila ninapoifanya kazi hii.

"Sikuchagua kazi hizi kwa kuwa sikuwa na uwezo wa kufanya kazi nyingine, nasema uwezo ninao, tena sana, lakini napenda kumtukuza Mungu,"anasema.Anasema kuwa siku zote amekuwa akiamini kazi hiyo anayoifanya ina uwezo wa kuwasaidia watu wengi, ingawa si kwa kuwasaidia kifedha kama wanavyodhani au kutaka watu wengi, bali inaweza kuwasaidia kiroho zaidi.Anashukuru kuona kuwa kazi yake imewasaidia watu wengi, hasa kwa kuweza kuwabadilisha maisha yao, kiroho zaidi na kuwaondoa katika mazoea na tabia mbaya.

"Wapo watu ambao hutoa msaada wao kwa njia ya pesa na mali, lakini mimi nimeamua kutoa msaada huo kwa njia ya kuwakomboa watu kupitia neno la Mungu na nina furaha sana kuona angalau nimefanikiwa,"anasema kwa furaha mwanamama huyu.Lakini, pamoja na kufanya kazi zake za kila siku, anasema kuwa alikuwa akiendelea na kazi ya kuimba akiwa mwimbaji binafsi (solo artist). Anaongeza kwamba siku zote alikuwa akipenda sana kuimba, hasa nyimbo za Injili.

Tangu azame katika fani hiyo, Ency anasema kuwa ameshiriki kutunga na kuimba nyimbo nyingi akiwa ametunga nyimbo nyingi.Anazitaja baadhi yake kuwa ni, Tanzania ni nchi yetu,Tanzania njoo kwa Bwana,Hapo mwanzo neno moja na nyingine nyingi ambazo zinahamasisha watu kutambua uwezo wa Mungu katika kusaidia watu wake.

Anasema kuwa kila siku, yeye hufurahi kuona shughuli yake anayofanya ya uimbaji wa nyimbo za Injili inakua na kupata umaarufu.Anaongeza kuwa siku zote amekuwa akipenda sana kumtukuza Mungu na kuamini kuwa ndiye msaidizi wake katika karibu kila jambo, kwani anaamini kila alifanyalo ni kwa uwezo wa Mungu na hakuna atakaloweza kulifanya bila msaada wake (Mungu).

"Si kama nilishindwa kwenda kufanya kazi nyingine zozote. La hasha! Uwezo na akili nikiwa shuleni nilikuwa nao na hadi sasa ninao na ningeweza kusoma somo lolote na nikafaulu, ila kazi ninayoifanya ni ya wito zaidi, "anasema.Anasimulia kuwa akiwa shuleni sikuzote alikuwa anao uwezo sana darasani kimasomo na ndio maana aliweza kufaulu masomo yake tangu shule ya msingi hadi chuo na kama angetaka angeweza kujiendeleza zaidi kimasomo."Laiti ningetaka ningejiendeleza kwa masomo mengine kama ya uhasibu, udaktari na mengineyo, lakini nikaamua kujielekeza zaidi katika kumtukuza Mungu," anaeleza.

Anaongeza kuwa amekuwa akiamini kuwa binadamu awapo duniani ni vizuri kujitahidi kufanya kazi yoyote au kitu ambacho moyo wako unakipenda na kamwe asifanye kazi kwa kuwa eti fulani anaifanya.Kwa hilo, msanii na mwanamama huyo anasema itakuwa sawa na kuunyayasa moyo wako na kutoutenda haki, pengine hata mbele za mwokozi.Anasema kuwa na ndoto yake na kutaka kuitimiza kumechangia kwa kiasi kikubwa katika kufanikiwa kwake. Anawashukuru wazazi wake kwa kumruhusu kufikia azma yake, hasa baada ya kuchagua kazi ya kufanya.

Anawashauri wazazi wawasimamie watoto wao katika kuchagua aina ya kazi za kufanya, isipokuwa wawape uhuru wa kuchagua nini wanataka kusomea au kufanya kwa ajili ya maisha yao ya baadaye.Hata hivyo, anaeleza mshangao wake hasa kwa baadhi ya watu, hasa akinamama ambao wanadiriki kufanya vitu ambavyo hawana uwezo navyo. Anaeleza kuwa kutokana na baadhi yao kuiga kwa ajili siyo ya kufanikiwa, au kwa sababu tu fulani anafanya hivyo, imesababisha wengi wao kushindwa kufanikiwa.Anakiri hata hivyo kwamba kila mtu duniani ana wito wake wa kufanya kitu, lakini kama mtu atakuwa anapenda kufanya vitu kwa kuiga au kwa vile wanafanya hivyo wengine, si vizuri.Hadhani kuwa hilo linafanyika kwa kwa ajili ya kujiletea maendeleo, akiamini kuwa kila siku mtu akitaka maendeleo hapaswi kulazimisha kitu kwa nguvu.

"Kwa watu wanofanya biashara usione mwenzako anafanya biashara hata za mamilioni ya fedha nawe ukataka kufanya hizo hizo biashara, angalia kwanza unao uwezo katika biashara na kama huwezi basi fanya kitu kitu kingine kulingana na uwezo wako na maendeleo yatakuja taratibu,"anashauri.Msanii huyo anasema kuwa ndiyo maana anashiriki kazi ya muziki huu wa Injili, siku zote akiamini kuwa ndiyo kazi ya wito wake na kamwe hafikirii kuiacha au kujiondoa.Hata hivyo, anasema kuwa hapendi tabia ya wasanii na waimbaji wengine kuchukulia uimbaji huo wa nyimbo na tungo za dini kama moja ya sehemu ya ajira tu, jambo ambalo anaamini kuwa huenda ikasababisha nyimbo hizo za injili kukosa thamani. Pia, jambo hilo halileti picha nzuri, hasa ikizingatiwa kuwa Injili ni neno la Mungu."Unajua watu wanashindwa kuelewa kuwa uimbaji ni wito na si biashara kama wafanyavyo wengine na pia ni dhambi kuifanya Injili kuwa kitegauchumi, bila kuiishi na kutegemea kuchuma tukupitia nyimbo hizo za injili tu,"anasema.

Anaamini kuwa wapo baadhi ya wasanii ambao wana mtazamo kama huo na hao ndio wanapotosha maana halisi ya muziki huo. Kwa mtazamo wake, anasema kuwa analaani tabia kama hiyo kwa vile si tu kudhalilisha nyimbo muziki au nyimbo za injili, pia inamdhalilisha hata mwimbaji mwenyewe.Anasema kuwa haileti picha nzuri kwa mfano mtu unapokutana na mwimbaji wa nyimbo za injili au hata kumwona akiwa yupo katika mazingira mabaya na pia katika mavazi yasiyo na muonekano mzuri mbele za watu."Nashauri kwamba uimbaji huu wa muziku wa Injili usiishie tu katika burudani, bali uimbaji huu uwe kwa lengo la kutangaza neno la Mungu na watu waweze kubadilika kwa kupitia uimbaji huu," anaonya.Anaongeza kuwa kitu cha kushangaza hasa siku hizi ni kuona nyimbo za Injili zimekuwa ni kama sehemu ya burudani na kuwakuta watu wanaburudika nazo na kisha kuacha hapo hapo, kitu ambacho anasema kuwa si lengo la muziki huo, ambao unajielekeza zaidi katika kusaidia watu watu kubadilika kupitia sanaa hiyo iliyomo katika neno la Mungu.

Anasema kuwa yeye anapokuwa anaimba nyimbo jukwaani, kwake nyimbo hizo za Injili, lengo lake si kuwaelekeza watu kaitka kupata burudani na kisha kuondoka, bali ni kwa lengo la watu kupata ujumbe,kuelewa na kisha kuufanyia kazi kwa kujua ni nini wanatakiwa wafanye.Mwanamama huyo ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Woman of Wisdom Trust Fund, shirika linalojihusha na kuwasaidia watoto yatima na wasio jiweza anasema jamii inatakiwa kuwajali watu hao.Anasema kuwa kikundi chake hicho kinasaidia watoto 20 wanaosaidiwa kwa kusomeshwa na pia kupata mahitaji mengine katika maisha. Ili kutimiza azma hiyo, Mwalukasa anasema wamekuwa wakiandaa matamasha mbalimbali kwa ajili ya kusaidia watu wasiojiweza.

Kwa upande wa kazi yake, hivi karibuni alizindua albamu yake ijulikanayo kama, Nakuhimidi ambayo aliizindua katika ukumbi wa Land Mark Hotel , Ubungo jijini Dar es Salaam. Anakiri kuwa uzinduzi huo ulikuwa wa aina yake baada ya kuhudhuriwa na watu wa rika tofauti tofauti.Anasema kuwa fedha zilizopatikana kutokana na tamasha hilo zilitengwa kwa ajili ya kusaidia watu wasiojiweza na yatima ambao ndio walengwa katika mfuko wake.Anaamini kuwa Watanzania ni watu wenye upendo na umoja, hivyo ni lazima waweze kuonyesha upendo huo kwa watu hasa wale wanohitaji msaada kwa kuwapatia msaada hata kama ni mdogo.

Anasema kuwa kutoa msaada kwa wasiojiweza haimaaanishi uwe na uwezo mkubwa kwani hata kama una uwezo mdogo, mtu anaweza kuonyesha upendo huo kwa kutoa msaada kulingana na uwezo. "Tatizo watu wameweka fikra kwamba wasiojiweza wanatakiwa kusaidiwa na mashirika tu kitu ambacho si cha kweli kwani hata mtu mbinafsi unaweza kuonyesha upendo wako kwa kuwasaidia watu hawa,"anasema.Anakariri usemi wa wahenga usemao, 'kutoa ni moyo na si utajiri' na kuongeza kuwa umefika wakati kwa kila Mtanzania kutoa ushirikiano kwa watu hao ambao maisha yao yanawategemea wengine."Binafsi huwa inaniuma sana nikipita barabarani au mitaani, nikakutana na watoto wadogo wakiomba, hawa hawana mtu wa kuwasaidia na wakati huohuo wapo watoto wa umri kama wao hawako shuleni, jamani tuwasaidie,"anamalizia.


[Makala hii ni kwa mujibu wa mtandao wa  Habari Tanzania]

Saturday, October 8, 2011

JACQUELINE WOLPER: Kutoka saluni hadi uigizaji nyota



 
‘UKIONA vyaelea, vimeundwa’ huu ni moja kati ya misemo iliyopo katika lugha ya Kiswahili ambayo inalenga kuonesha kuwa kila king’aacho au kila chenye mafanikio, kina mwanzo wake.

Usemi huu utaweza kuakisi tasnia ya filamu hapa nchini ambayo baadhi ya wasanii wake wanang’ara na kuwa na mafanikio hivi sasa, lakini wakiwa na historia ya kuanza mikikimikiki mbali huku wakipitia mabonde na milima.

Baadhi ya wasanii ambao kwa sasa wanang’ara lakini wamepita safari ndefu ni Steven Kanumba ‘Kanumba’, Vicent Kigosi ‘Ray’, Jacob Steven ‘JB’, Yvonne Cherrie ‘Monalisa’, Lucy Komba na wengineo wengi.

Lakini pia wapo walioanza kuibuka ndani ya miaka takribani mitano iliyopita lakini kwa sasa wamekuwa tishio katika fani hiyo, mmojawapo ni msanii Jacqueline Wolper, ambaye karibu miaka minne, amekuwa mwigizaji nyota wa filamu kutokana na kazi zake kukubalika ipasavyo.

Akizungumza katika mahojiano na HABARILEO Jumapili, Jackline ambaye anazungumza taratibu na kwa kituo na kama ni mtu wa kukurupuka unaweza kumdhania kuwa ana maringo, anaeleza nia yake ya kutaka kuwekeza katika fani hiyo ikiwa ni pamoja na kuwasaidia wasanii wachanga.

“Pamoja na mafanikio niliyoyapata ndani ya miaka minne, nina kiu ya kujidhatiti katika fani hii. Kiu yangu ni kuhakikisha nafungua kampuni kubwa ya kuuza vifaa vinavyotumika katika filamu, usambazaji wa kazi za filamu na kuanzisha kikundi cha sanaa.

“Napenda sana kuwasaidia na kuwainua wasanii chipukizi kama mimi nilivyoinuliwa, na njia pekee ni kuwa na kikundi amchacho ndicho kitakachokuwa chimbuko la kuibua vipaji vya uigizaji,” anasema.

Jacqueline ambaye pia anapendelea kucheza mpira wa pete (netiboli) anasema kwa mwaka mmoja ameweza kutoa filamu zake zipatazo tatu, huku kazi zake zikisimamiwa na Meneja wake Leah Richard. a.k.a Lamata, ambaye pia ndiye mtunzi wa kazi yake.

Kazi hizo ni Candy, Time After Time na By Princes. Mafanikio hayo ya Jacqueline hayakuja hivi hivi bali yalianzia mwaka 2008 kwa mara ya kwanza aliposhirikishwa kwenye filamu ya kwanza na msanii Lucy Komba kwa kupewa nafasi ya kuigiza katika filamu ya ‘Ama Zangu Ama Zao’, kama Katibu Muhtasi.

Anasema kazi nzuri aliyoifanya baada ya kutambuliwa na aliyekuwa jirani yake (Lucy) aliungwa mkono na kuelekezwa vitu vingi na msanii huyo mzoefu na aliyecheza filamu nyingi za ‘Kipenzi Changu’, Surprise, ‘Red Valentine’ na ‘Family Tears’, ambazo ziliteka soko na kumfanya ajulikane.

Baadaye alitunga filamu zake mbili ya ‘Wekeend’ na ‘My Princess’ ambazo zilifanya vizuri sokoni na akapata moyo wa kuwa mwigizaji rasmi. Filamu nyingine alizoigiza ni ‘Utumwa wa Mapenzi’ na ‘All About Love’ iliyotungwa na Jennifer Kiaka ‘Odama’, ambayo anasema aliipenda kutokana na kuvaa vyema uhusika kwa kuwa aliigiza kama mtoto.

“Filamu ya All About Love ndio filamu niliyoigiza na hata nikiiangalia nakubali kazi niliyoifanya, vile vitu nilivyoigiza asilimia kubwa niliigiza vitu vyangu vya kweli,” anasema. Jacqueline pia anasema filamu iliyomsisimua sana tangu awe msanii ni ‘Last Minutes’ ya Leah, ambayo alicheza na Bajomba.

“Naipenda na huwa nairudia kuitazama kwa sababu inaelimisha, kuna siku wakati natoka super market (dukani) kuna mtu mmoja alilia baada ya kukutana na mimi mlangoni alisema niliigiza maisha yake, lakini bahati nilikuwa pamoja na mtunzi (Lamata) alimuelewesha kuwa hakumtungia mtu kisa kile.

“Lakini pia kuna filamu ya Candy ilikuwa na ugumu wake katika kuigiza hasa kutokana na kuvaa uhusika wa mtu mwenye ugonjwa wa akili ‘chizi’. Kwa watu wengine itakuwa ngumu, lakini kwasababu mimi nina kipaji niliweza.

Nafasi ambazo naweza kuvaa uhusika kikamilifu ni pamoja na kuwa chizi na mtu anayeteswa,” anasema. Jacqueline anasema licha ya kujikita kwenye uigizaji filamu kwa miaka michache, amekuwa nyota anayekabiliwa na migogoro mingi, ambayo anadai haipendi kwa vile si tabia yake.

Anasema anapenda kuelewana, kucheka na kila mtu na hata kubadilishana mawazo, lakini anajuta kwa jinsi umaarufu unavyomuingiza katika matatizo na watu mbalimbali na kuwa wengine wamekuwa wakimfikiria visivyo.

“Ndiyo inatokea hivyo na wakati mwingine magazeti huwa yanaandika tu, na ndiyo yamekuwa chanzo kikubwa cha kutukatisha tamaa. Pia wapo wengine wanataka kukusema vibaya hata kama hakufahamu, wengine wanaweza kuamini kuwa mimi nina tabia mbaya lakini bila kujua ukweli wangu, mimi siko hivyo,” anasema.

Msanii huyo ametoa changamoto kwa wasanii wenzake wa filamu, wasiendekeze migogoro kwa vile haina manufaa yoyote badala yake wajidhatiti katika fani ili kuendeleza sanaa hiyo ambayo anasema sasa imekuwa na soko kubwa ndani na nje ya nchi.

Anapozungumzia tasnia ya filamu hapa nchini, Jacqueline anasema: “Kinachotakiwa hapa ni kwa wazalendo kuwekeza katika fani hii, filamu zetu ziko juu na hata uwezo wetu wa kuigiza uko juu pia, kinachozuia sanaa kuonekana haina maslahi ni ukosefu wa fedha.

Kwa hakika ukitulinganisha sisi na Wanigeria hakika sisi tuko juu, vikwazo vikiondoka mambo yote yatakuwa sawa.” Jacqueline anasema kujitokeza wageni wengi kuwekeza mitaji yao katika filamu, kunamaanisha kuwa ina faida, na anawataka wazawa kuingiza mitaji yao ili kuongeza ushindani wa malipo kwa wasanii na kuondoa unyanyasaji uliokithiri.

“Kampuni zinazojihusisha na masuala ya kutengeneza filamu na kusambaza ni chache na karibu zote zinashikwa na Waasia, tunataka na Watanzania wengine waweke mitaji yao ili tulipwe vizuri na kutuinua sisi wasanii wa filamu,” anasema.

Akizungumzia manufaa aliyopata katika maisha yake tangu awe msanii wa filamu, anasema ukiachia mbali umaarufu alionao kutokana na tasnia hiyo kutoa nafasi kwake kufahamiana na watu wengi, lakini amenufaika kwa vingi ambavyo amedai ni siri yake.

Jacqueline anasema pamoja na unyonyaji wanaofanyiwa katika filamu, anamshukuru Mungu kwa alichopata maishani mwake, ambapo amekiri wasanii wenye majina makubwa angalau wanaambulia kitu kuliko chipukizi.

“Kwa sisi ambao tayari tuna majina makubwa kidogo alhamdulilah, lakini kwa chipukizi ndiko kuna kilio kikubwa sana kama cha hakimiliki kwani imekuwa vigumu kudhibiti na nadhani hili tatizo halitakwisha vizazi na vizazi,” anasema msanii huyo.

Akizungumzia wasanii wenye uwezo mkubwa, Jacqueline anasema kwanza anajipenda yeye mwenyewe kutokana na uwezo wake katika kuuvaa uhusika, halafu Irene Uwoya kutokana na kufanana naye na pia uwezo wake katika uigizaji ambao alisema anaukubali.

Nje ya nchi anasema anampenda msanii nyota wa filamu wa Marekani, Halle Berry kwa alivyo mtulivu katika uigizaji na msafi.

Jacqueline alizaliwa Moshi Mjini mwaka 1988 na alimaliza elimu ya msingi wilayani Mwanga mwaka 2000 katika Shule ya Msingi Mawenzi, na baadaye kusoma shule za sekondari tofauti za Magrath, Ekenywa lakini aliishia kidato cha tano katika shule ya Masai mwaka 2007 na baada ya hapo hakuendelea na masomo ya sekondari kutokana na sababu ambazo hakutaka kuzitaja.

Baadaye alijiunga na Kozi ya Lugha katika Chuo cha ICC Arusha na kwenda kujiunga na Chuo cha USA Contact na kuhitimu Stashahada ya Masoko na Biashara na kuajiriwa na kampuni hiyo kwa muda mfupi kabla ya kuacha na kuanzisha biashara ya saluni.

“Nilianzisha saluni pale Mwenge, ile bomoabomoa ya kwanza ilinikuta na nikaamua kuihamishia Kijitonyama ambako pia niliamua kuifunga baada ya kuchagua kuendelea na fani ya uigizaji,” alisema Jacqueline ambaye anasema bado anafanya biashara ndogondogo hadi sasa.

Jacqueline anamaliza kwa kusema: “ Kufika kwangu hapa nina watu wa kuwashukuru, kwanza ni Lucy Komba, Ray (Vicent Kigosi), Kanumba (Steven Kanumba) na Mtitu Game.
[Makala hii ni kwa mujibu wa gazeti la Habari Leo la tarehe 08 Oktoba 2011]

Friday, August 12, 2011

Je Wajua kuwa machungwa ni zao la matunda linalovunwa sana duniani?

CHUNGWA ni tunda la msimu. Ni kati ya matunda yanayovunwa sana duniani. Jina la kisayansi ni Citrus aurantium L. var. sinensis L. au Citrus sinensis (L.) Osbeck.

Tunda lenyewe ni kijani na rangi inabadilika kuelekea njano likiiva. Pamoja na limau, danzi, balungi na ndimu ni mojawapo kati ya matunda chungwa. Siku hizi ni tunda linalovunwa zaidi kati ya matunda chungwa.

Asili yake ni katika Asia ya Kusini-Mashariki ambako lilioteshwa na wakulima. Kuna aina mbili yanayotofautiana kwa ladha ama chungu au tamu. Lenye ladha chungu liliwahi kusambaa duniani hivyo jina la Kiswahili limetunza ladha hii hata kama matunda mengi yanayopandwa siku hizi ni aina tamu.

Chungwa tamu lilisambaa kote duniani baada ya Wareno kuchukua machipuko yake na kuyapanda kwanza Ureno baadaye hata Amerika na Afrika kuanzia karne ya 15. Chungwa, na hasa chungwa tamu, ni jamii ya matunda ya citrus, na huaminika kuwa yalikuzwa miongoni mwa enzi za pomelo na tangerine.

Mti wake mdogo utoao maua hufikia urefu takribani mita kumi na majani yake yasiyokauka muda wote. Machungwa asili yake ni huko kusini mwa Asia. Tunda lifahamikalo kisayansi kama citrus sinesis huitwa chungwa tamu ili kutofautisha na citrus aurantium, chungwa chungu.

Matunda yote jamii ya jenasi ya citrus, huzaliana na familia yao hujumuisha machungwa, ndimu na limao. Matunda ya jamii hii huonwa kama ni ya aina ya beri sababu ya kuwa na mbegu nyingi, kuwa laini na nyama nyingi huku yakikua kutoka kwenye ovari moja.

Kama ilivyo kwa jamii ya matunda ya citrus, machungwa nayo huwa na hali ya asidi, yenye kiwango cha pH karibu na 2.5 -3, kulingana na umri wake, ukubwa na aina ya chungwa. Japo si kama ilivyo kwa limao, bado machungwa huwa na kiwango cha asidi cha kutosha, sawa kabisa na hata siki ya nyumbani.

Machungwa kwa kawaida hulimwa kwa ajili ya biashara na hulimwa maeneo mengi duniani. Wazalishaji wa machungwa wanaoongoza duniani ni Brazili, Marekani na Meksiko. Machungwa huathirika kwa haraka sana na ukungu hivyo huhitaji matunzo mazuri pindi joto dogo sana linapotegemewa.

Michungwa huweza kukuzwa maeneo yenye joto na hata yale yenye baridi. Kama ilivyo kwa matunda mengine ya citrus, ili kupata mazao mazuri haina budi kukuza michungwa katika joto la nyuzijoto 15.5 °C - 29 °C.

Miti ya machungwa iliooteshwa kutokana na mbegu zilizonunuliwa madukani inaweza kuwa tofauti kabisa na ile miti ya asili iliyozalisha mbegu hizo. Hii hutokana na mabadiliko ya kizazi yanayotokana na kuchanganywa mbegu kisayansi kwa muda mrefu.

Ili kupata mmea wa mchungwa kama tunda ambalo linanunuliwa, huna budi kuitunza mbegu hiyo kwenye unyevunyevu kisha tu baada ya kuzitua kwenye tunda na kuziotesha katika hali ya unyevu; na pindi mmea uchipuapo hapo ukapandwe kwenye udongo kusudiwa.

Machungwa yanakuzwa katika hali mbalimbali za joto duniani kote, na ladha yake hubadilika kuanzia hali ya utamu mpaka uchungu kabisa. Tunda kwa kawaida humenywa na kuliwa au huminywa na sharubati yake kunywewa.

Limezungukwa na ganda lenye ladha chungu lakini huweza kukamuliwa na kuondolewa maji yake na kutumika kwa chakula cha mifugo. Pia, hutumika kuongeza ladha ya vyakula vingine na hata maganda yake hufaa kwa kazi hii.

Sehemu nyeupe ya ndani, kati ya nyama na ganda la nje nayo huwa na vitamini sawa kabisa na nyama ya ndani. Sharubati ya machungwa ndiyo bidhaa kuu kuliko zote ya machungwa. Huweza kuzalishwa kwa matumizi ya nyumbani lakini hasa hufanywa kwa minajili ya biashara.

Sharubati ya kugandishwa ya machungwa hutengenezwa kutokana na majimaji ya machungwa pia. Mafuta ya machungwa ni bidhaa ndogo inayotengenezwa kwa kukamua maganda ya machungwa. Hutumika kwa kuongeza ladha ya chakula na zaidi kwenye utengenezaji wa manukato.

Maua ya machungwa nayo hupendwa kwa harufu yake nzuri na hutumika mara nyingi nyakati za harusi na huhusishwa na bahati njema. Majani ya michungwa yanaweza kutumika kutengenezea chai.

Licha ya kwamba zao hili hufahamika duniani kutokana na mahitaji yake, lakini bado halijapewa kipaumbele nchini hasa kutokana na wakulima kutokuwa na uhakika wa soko kwa ajili ya bidhaa zao.

Serikali inahitajika kuwafikiria na kuwapa mbinu za kuweza kuboresha kilimo chao ili waweze kuvuna matunda mengi yanayohitajika. Ni wazi kwamba kuna wakulima wachache ambao wamepata fursa ya kufanya kazi na kampuni mbalimbali ambazo hutengeneza bidhaa za matunda, hao ndio wanaonufaika.

Lakini pia wapo ambao wana moyo ya kulima machungwa kwa wingi lakini wanaendelea kukandamizwa na wafanyabiashara wakubwa ambao huwanunuza katika mashamba. Wakulima wengi hawana vikundi vya ushirika kwani wengi hufanya kazi kwa kujitegemea.

Hiyo ni changamoto kubwa inayomfanya aendelee kukandamizwa na mfanyabiashara mkubwa. Wangekuwa na vikundi ni wazi kwamba hata bei wangejipangia wenyewe na wangekuwa na uwezo wa kusafirisha sokoni na kuuzwa kwa bei wanayotaka.

Machungwa huoza haraka. Wakati mwingine wakulima wanapata hasara kubwa hasa pale ambapo wanasubiri usafiri wa kupeleka bidhaa zao sokoni, kuna maeneo mengine barabara sio nzuri, hivyo mpaka yafike sokoni mengi yanakuwa yameoza.

Bado hawana uelewa wa kutosha ni kwa jinsi watahifadhi matunda yao yasiweze kuharibika mapema. Hiyo ni changamoto kubwa inayowakumba wakulima na wafanyabiashara wa machungwa. Kwani baadhi yao wamekuwa wakihifadhi ilimradi wanavyojua wao.

Pia, wafanyabiashara na wakulima wa machungwa hupenda kurundikana sehemu moja wakati wa msimu wa machungwa hivyo pia, biashara kuwa ngumu kwa vile wanauza kiushindani. Zipo sehemu nyingi ambazo wanaweza kufanya biashara zao na zikatoka.

Hufahamika kuwa, siku zote mazao ya mboga na matunda yana thamani kubwa kuliko mazao mengine na yanahitaji uangalifu mkubwa zaidi wakati wa uzalishaji. Udhibiti wa visumbufu vya mazao hayo wakati yakiwa shambani ni muhimu ufanyike kwa wakati unaotakiwa na kwa ufanisi ili kuleta matokeo mazuri katika uzalishaji.

Mazao ya matunda yaliyo machache na hafifu kutokana na uzalishaji duni huwa na faida ndogo ambayo inakatisha tama katika kuwekeza wakati wa kutumia teknolojia za utunzaji bora na usindikaji na hifadhi.

Ili kupata mazao bora na kupunguza uharibifu, mkulima hana budi kuzingatia kanuni za kilimo bora cha matunda pamoja na mbinu bora za uvunaji, utayarishaji na uhifadhi. Mbinu hizi zinahusisha pia usindikaji wa mazao hayo wenye lengo la kuongeza ubora na kuhifadhi kwa muda mrefu kwa ajili ya masoko na kuwezesha upatikanaji wakati wote.

(Makala kwa mujibu wa mtandao wa gazeti la Habari Leo Agosti 2, 2011)

Wednesday, August 10, 2011

BIASHARA YAKO NI NINI? Utalijibuje swali hili?

BIASHARA YAKO NI NINI?

Unaweza ukajibu swali hili kwa kuangalia vitu viafutavyo nini unazalish na kwa ajili ya nani?
Maana yake ni kuwa biashara ina mambo mawili
Uzalishaji (Production)
Masoko (Marketing)
Kitu cha msingi kukumbuka uko katika biashara ili kuzalisha /kutafuta pesa.
Maana yake ni kuwa lazima uwe na vitu vya kuuza na pia lazima uwe na watu wa kununua hivyo vitu vyako(kwa maana nyingine ni lazima uwe na bidhaa/huduma na pia wawepo wanunuzi wa bidhaa zako.)
Kupata vitu unavyotaka kuuza unahitaji uzalishaji (bidhaa/huduma) na pia kutafuta masoko ya kuuzia hizo bidhaa/huduma ulizozalisha.
Kwa hiyo biashara kwa maana nyingine ni bidhaa/huduma na masoko.
Tuanze na uzalishaji (Production)
Mfano fikiria
Kama wewe ni mtengenezaji wa viatu/miwani ya jua, ukiulizwa biashara yoko ni nini , utasema ni kutengeneza miwani /viatu.lakini hii ni biashara yako kweli?
Unachotengeneza ndicho unachauza?
Kama unatengeneza miwani ya jua ,kutengeneza miwani ya jua sio njia pekee ya kuelezea uzalishaji wako.
Biashara yako ungeweza kuielezea kuwa ni kuzuia macho kupigwa na mionzi ya jua.
Kama utasema “nina biashara ya kutengeneza miwani ya jua” ni lazima utambue
Kuwa miwani ina vipande viwili vya plastiki vya rangi vilivyoshikwa na fremu za
Plastiki kwenye uso wako.
Hakuna mtu atakeye nunua miwani kwa kuwa anataka viande viwili vya plastiki/glasi vya rangi aviweke usoni mwake.
(HAPA NI LAZIMA UZALISHE ZAIDI YA MIWANI.)
Unapoelezea biashara yako lazima pia uelezee kuhusu masoko yake
(It’s marketing) mfano ;ukisema biashara yako ni kuuza miwani kwa waitali.
Kumbuka biashara ni uzalishaji na masoko.
Tuzumgumzie masoko (marketing)
“Utasema biashara yako ni biashara ya kutengeneza miwani za jua kwa waitalia”
Hii ni nzuri kidogo lakini kuna mamilioni ya waitalia , hakika huko katika biashara ya kuwatengenezea miwani za jua mamilioni ya waitali wote.
Fikiri biashara yako katika hali ya kwanini hawa watu wananunua miwani za jua?
Hapa biashara yako itakuwa “kutengeneza miwani ya jua ambayo inazuia mionzi kwa ajili ya waitalia wanopenda usalama wa macho yao"
Mfano ukisema biashara yako ni kuzalisha fulana za kampuni ya ukwamba ;
Ukwamba akakupatia kila kitu (malighafi zote ) kwa ajili ya uzalishaji na aina ya fulana ,mfano na ukubwa wa hizo fulana. Hapa maana yake ni kwamba ukwamba anahitaji uweke gharama za uzalishaji tu hasa wafanya kazi (labour costs)
Je unafikiri biashara yako ni nini?
Je kampuni ya ukwamba kiuhakika inanunua nini hasa kutoka kwako?
Je ni bei rahisi ya ufanyajikazi wako?(low cost of your labour).


Muhimu;
Kama hutasimamia vizuri bishara yako/kampuni yako au utachelewesha mzigo, mzigo ukawa chini ya kiwango,ukubwa tofauti, rangi tofauti na mlivyokubaliana, Ukwamba hata nunua huduma toka kwako hata kama una bei rahiasi kuliko kampuni yoyote hapa duniani.
Kutokana na maelezo hayo unaweza kusema biashara yako ni kutoa huduma (services) kuliko kutengeneza bidhaa.
Japokua unampatia ukwamba bidhaa za fulana,lakini ukwamba anapenda au anavutiwa na huduma yako ya usimamizi wa uzalishaji.
Biashara yako hapa ni kuuza utaalam wako wa usimamizi wa uzalishaji kwa kampuni ya ukwamba.(selling production management skills)
“Unachozalisha kinaweza kuwa sicho unachokiuza”


Ili kufafanua vizuri kuhusu mada hiyo hapo juu hebu jaribu kufikiria kuhusu magazeti
Magazeti yanauza nini?
Unaweza kufikiri na kusema kuwa magezeti yanauza habari kwa jamii,
Lakini jiulize mwenyewe kuuza magazeti kutaweza kuzalisha hela za kutosho kuendesh kampuni? Hela itakayopatikana haitoshi, kwani kuchapisha nakala moja
bei yake ni mara mbili ya bei ya kuuzia gazeti.
Hapa makampuni ya magazetai yanauza nafasi za matangazo.
Na ndio chanzo kikibwa cha mapato yao.
(They produce what they don’t sale and they sale what they don’t produce)


Muhimu;
Kama utashindwa kujua hasa kampuni yako iko katika biashara gani /inauza nini/
Inazalisha nini utakuwa umepoteza mwelekeo na hutatengeneza faida ambayo ndio msingi wa kuwa katika biashara (money making)


Hitimisho
1. unachozalisha/unachotengeneza kinaweza kuwa sicho unachouza.
Kujua uko katika biashara gani au nini biashara yako lazima ufikirie haya;
Kwa nini wananunua toka kwako?
2. wakati unafikiria kuhusu nani watanunua kutoka kwako ,fikiria pia kuhusu nani anahusika katika mafanikio yako ya kifedha ya kampuni
Watanzania wengi hatujui hasa ni nini biashara zetu(what is the business of your enterprise) hii inasababisha watu wengi sana kupata hasara na kufunga baadhi ya makampuni yao.

Ahsanteni sana
Karibuni wadau wote kwa maoni na ushauri.
source www.jamiiforums.com

Biashara Yako Ni Nini?

BIASHARA YAKO NI NINI?

Unaweza ukajibu swali hili kwa kuangalia vitu viafutavyo nini unazalish na kwa ajili ya nani?
Maana yake ni kuwa biashara ina mambo mawili
Uzalishaji (Production)
Masoko (Marketing)
Kitu cha msingi kukumbuka uko katika biashara ili kuzalisha /kutafuta pesa.
Maana yake ni kuwa lazima uwe na vitu vya kuuza na pia lazima uwe na watu wa kununua hivyo vitu vyako(kwa maana nyingine ni lazima uwe na bidhaa/huduma na pia wawepo wanunuzi wa bidhaa zako.)
Kupata vitu unavyotaka kuuza unahitaji uzalishaji (bidhaa/huduma) na pia kutafuta masoko ya kuuzia hizo bidhaa/huduma ulizozalisha.
Kwa hiyo biashara kwa maana nyingine ni bidhaa/huduma na masoko.
Tuanze na uzalishaji (Production)
Mfano fikiria
Kama wewe ni mtengenezaji wa viatu/miwani ya jua, ukiulizwa biashara yoko ni nini , utasema ni kutengeneza miwani /viatu.lakini hii ni biashara yako kweli?
Unachotengeneza ndicho unachauza?
Kama unatengeneza miwani ya jua ,kutengeneza miwani ya jua sio njia pekee ya kuelezea uzalishaji wako.
Biashara yako ungeweza kuielezea kuwa ni kuzuia macho kupigwa na mionzi ya jua.
Kama utasema “nina biashara ya kutengeneza miwani ya jua” ni lazima utambue
Kuwa miwani ina vipande viwili vya plastiki vya rangi vilivyoshikwa na fremu za
Plastiki kwenye uso wako.
Hakuna mtu atakeye nunua miwani kwa kuwa anataka viande viwili vya plastiki/glasi vya rangi aviweke usoni mwake.
(HAPA NI LAZIMA UZALISHE ZAIDI YA MIWANI.)
Unapoelezea biashara yako lazima pia uelezee kuhusu masoko yake
(It’s marketing) mfano ;ukisema biashara yako ni kuuza miwani kwa waitali.
Kumbuka biashara ni uzalishaji na masoko.
Tuzumgumzie masoko (marketing)
“Utasema biashara yako ni biashara ya kutengeneza miwani za jua kwa waitalia”
Hii ni nzuri kidogo lakini kuna mamilioni ya waitalia , hakika huko katika biashara ya kuwatengenezea miwani za jua mamilioni ya waitali wote.
Fikiri biashara yako katika hali ya kwanini hawa watu wananunua miwani za jua?
Hapa biashara yako itakuwa “kutengeneza miwani ya jua ambayo inazuia mionzi kwa ajili ya waitalia wanopenda usalama wa macho yao"
Mfano ukisema biashara yako ni kuzalisha fulana za kampuni ya ukwamba ;
Ukwamba akakupatia kila kitu (malighafi zote ) kwa ajili ya uzalishaji na aina ya fulana ,mfano na ukubwa wa hizo fulana. Hapa maana yake ni kwamba ukwamba anahitaji uweke gharama za uzalishaji tu hasa wafanya kazi (labour costs)
Je unafikiri biashara yako ni nini?
Je kampuni ya ukwamba kiuhakika inanunua nini hasa kutoka kwako?
Je ni bei rahisi ya ufanyajikazi wako?(low cost of your labour).


Muhimu;
Kama hutasimamia vizuri bishara yako/kampuni yako au utachelewesha mzigo, mzigo ukawa chini ya kiwango,ukubwa tofauti, rangi tofauti na mlivyokubaliana, Ukwamba hata nunua huduma toka kwako hata kama una bei rahiasi kuliko kampuni yoyote hapa duniani.
Kutokana na maelezo hayo unaweza kusema biashara yako ni kutoa huduma (services) kuliko kutengeneza bidhaa.
Japokua unampatia ukwamba bidhaa za fulana,lakini ukwamba anapenda au anavutiwa na huduma yako ya usimamizi wa uzalishaji.
Biashara yako hapa ni kuuza utaalam wako wa usimamizi wa uzalishaji kwa kampuni ya ukwamba.(selling production management skills)
“Unachozalisha kinaweza kuwa sicho unachokiuza”


Ili kufafanua vizuri kuhusu mada hiyo hapo juu hebu jaribu kufikiria kuhusu magazeti
Magazeti yanauza nini?
Unaweza kufikiri na kusema kuwa magezeti yanauza habari kwa jamii,
Lakini jiulize mwenyewe kuuza magazeti kutaweza kuzalisha hela za kutosho kuendesh kampuni? Hela itakayopatikana haitoshi, kwani kuchapisha nakala moja
bei yake ni mara mbili ya bei ya kuuzia gazeti.
Hapa makampuni ya magazetai yanauza nafasi za matangazo.
Na ndio chanzo kikibwa cha mapato yao.
(They produce what they don’t sale and they sale what they don’t produce)


Muhimu;
Kama utashindwa kujua hasa kampuni yako iko katika biashara gani /inauza nini/
Inazalisha nini utakuwa umepoteza mwelekeo na hutatengeneza faida ambayo ndio msingi wa kuwa katika biashara (money making)


Hitimisho
1. unachozalisha/unachotengeneza kinaweza kuwa sicho unachouza.
Kujua uko katika biashara gani au nini biashara yako lazima ufikirie haya;
Kwa nini wananunua toka kwako?
2. wakati unafikiria kuhusu nani watanunua kutoka kwako ,fikiria pia kuhusu nani anahusika katika mafanikio yako ya kifedha ya kampuni
Watanzania wengi hatujui hasa ni nini biashara zetu(what is the business of your enterprise) hii inasababisha watu wengi sana kupata hasara na kufunga baadhi ya makampuni yao.
ahsante sana
karibuni wadau wote kwa maoni na ushuri.

source www.jamiiforums.com

Wese kama kawa: Wafanyabiashara ya Mafuta Wasalimu Amri.

Wafanyabiashara ya mafuta wasalimu amri  
Wednesday, 10 August 2011 23:47


KAMPUNI nne zilizopewa amri na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), ya kurejesha huduma hiyo mara moja za BP, Oilcom, Engen na Camel Oil zimesalimu amri na kuanza usambazaji na uuzaji wa mafuta katika vituo mbalimbali nchini.Hata hivyo, katika baadhi ya vituo jijini Dares Salaam, utoaji wa huduma hiyo ulikuwa kusuasua hali iliyowafanya baadhi ya vijana kufunga barabara na kuvizingira wakitaka kuhudumiwa kwa nguvu.Mbali ya kufunga barabara na kuzingira vituo, vijana hao pia walikuwa wakiandamana barabarani kuelekea kituo kimoja baada ya kingine hasa vile vilivyopo kando kando ya Barabara ya Mandela.

Polisi waingia vituoniPolisi jana walikuwa wakifuatilia kwa karibu usalama katika vituo vya kuuzia mafuta kwa askari wake kufanya doria vituoni.Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema kutokana na kauli ya Serikali, jeshi hilo limelazimika kulinda usalama na kukagua kuona ni vituo vilivyokuwa vikitii agizo hilo na vile vilivyokaidi.

“Hili suala linahitaji usimamizi wa hali ya juu, unajua tumelazimika kulinda usalama kwa wananchi kutokana na hizo foleni. Pia tunavikagua kujua kama vinatoa huduma,” alisema.

Camel wakutana lakini wauza mafuta
Mmoja wa maofisa wa Kampuni ya Camel ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini alisema wameanza kutekeleza amri hiyo na tayari malori yalianza kuchukua mafuta na kusambaza katika vituo.

Alisema kazi hiyo ilianza jana mapema asubuhi na kwamba sambamba na hilo, viongozi wa ngazi za juu walikuwa kwenye mkutano wa ndani kujadili namna ya utekelezaji wa agizo hilo.Waandishi wa gazeti hili walifika kwenye hifadhi ya kampuni hiyo, Kurasini na kushuhudia malori makubwa yakipakia shehena ya mafuta kupeleka vituoni.

Engen yajikosha kwa Serikali
Engen, baada ya Mkurugenzi wake, Selan Naidoo kutuhumiwa kuidharau Serikali kwa kuipa saa 24 ifidie hasara itakayopata kutokana na bei mpya elekezi, jana imeibuka na kusema kwamba imekuwa na uhusiano mzuri na Serikali ya Tanzania na wakati wote imekuwa ikishirikiana na taasisi mbalimbali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Wayne Hartmann wakati wote kampuni hiyo imekuwa na malengo chanya kwa Tanzania na kwamba msimamo utakuwa wa kudumu kwao kwa wakati wote watakaokuwa wakiendesha biashara ya mafuta nchini.

Alisema kauli iliyotolewa na Naidoo kuhusu bei mpya za mafuta zilizotangazwa na Serikali kuwa ni msimamo wa kampuni hiyo na haihusiani kwa namna yoyote na kampuni nyingine za mafuta nchini.

Hata hivyo, Hartmann alisema kuwa bei mpya za mafuta zilizoanza kutumika mwanzoni mwa mwezi huu, zimeyaweka makampuni ya mafuta katika wakati mgumu na mengi yamejikuta yakiuza kwa bei ya hasara.

Kwa upande wake Naidoo alisema vituo vingi vinavyomilikiwa na kampuni hiyo vingeanza kutoa huduma hiyo muda wowote kuanzia jioni kwa kuwa nyakati za mchana baadhi havikuweza kutoa huduma hiyo kwa kuwa havikuwa na mafuta.


Oilcom: Tumetekeleza maagizo
Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo ya Oilcom, Ahmed Bathawab alisema jana kwamba wametii agizo la Serikali na kusambaza mafuta kwenye vituo vyote vilivyopo chini ya kampuni hiyo.Alisema kampuni hiyo inasambaza mafuta kwa vituo zaidi ya 70 nchini kote, huku baadhi yake vikimilikiwa na kampuni hiyo na nyingine zikiwa chini ya washirika wake wa biashara.

Kuhusu agizo la kujieleza alisema wamepatiwa fomu na kujaza kisha kuzirudisha serikalini.“Tumetekeleza agizo la Serikali pamoja na masharti yake. Tumefungua vituo vyetu vya mafuta na kuhusu kujieleza walituletea fomu, tumejaza na kurudisha,” alisema Bathawab.Alisema kampuni yake imefungua vituo vyake 16 vya jijini Dar es Salaam na zaidi ya 70 vilivyopo nchi nzima na kueleza kwamba wamekubali kuuza kwa bei mpya iliyotangazwa na Ewura licha ya kulalamika kuwa ni bei ya hasara.

Alisema kampuni yake imekuwa ikipata hasara ya Sh117 kwa lita moja ya mafuta ya dizeli wakati hasara katika mafuta ya petroli ni Sh94.“Tumekubali agizo la Serikali siyo kutokana na amri yake pekee bali, hata sisi hatupendi nchi iingie kwenye matatizo. Tutaendelea kuuza kwa hasara hadi hapo tutakapofikia mwafaka,” alisema Bathawab.

Alisema pamoja na hatua hiyo bado wamiliki hao wanaendelea na mkutano na Ewura kujadili hatima ya sakata hilo.

BP yasuasua
Kwa upande wa Kampuni ya BP, jana walikuwa kwenye kikao kujadili agizo hilo la Serikali.Mwandishi wa gazeti hili alifika katika Ofisi za BP, Kurasini na kuelezwa kuwa viongozi walikuwa kikaoni na kwamba hakuna tamko ambalo lingetolewa mpaka kitakapomalizika.Mtumishi mmoja wa kampuni hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Agness Nsangalufu alisema: “Kwa sasa hivi hakuna taarifa yoyote kuna kikao kinaendelea labda nikupe namba ambayo ukipiga baadaye utapewa taarifa.”

Hata hivyo, namba hiyo ilipopigwa aliyepokea aliikata mara baada ya mwandishi kujitambulisha na haikupatikana tena hadi tunakwenda mitamboni.Mpaka saa 10 baadhi ya vituo kampuni hiyo vilikuwa havitoi huduma hiyo jambo lililoibua maswali mengi kutoka kwa wananchi hasa ikizingatiwa kwamba Serikali ina hisa katika kampuni hiyo.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Ewura, Titus Kaguo ilisema kampuni hiyo ilikuwa imetoa mafuta ya petroli lita 48,000 na dizeli lita 402,000 kwa ajili ya kuuzwa katika vituo vya rejareja.

Taomac yanywea
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Kampuni za Kuuza Mafuta Tanzania (Taomac), Salum Bisarara alisema hawezi kuzungumzia kauli iliyotolewa na Serikali juzi kwa sababu ilielekezwa kwa kampuni.

“Serikali jana (juzi) ilielekeza kauli yake kwa kampuni za kuuza mafuta, kwa sasa suala lolote linalohusu bei ya mafuta sisi hatuwezi kulizungumzia, suala hili linatakiwa lizungumzwe na kampuni, sisi haturuhusiwi kupigania mambo ya bei za mafuta kabisa,” alisema na kuongeza:

“Ewura wametutahadharisha tusije tukavunja sheria kwa sababu suala hili limefika pabaya, hata suala la adhabu haturuhusiwi kulizungumzia.”

Mapema wiki hii Ewura iliweka bayana kwamba ingeishauri Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC) kuifuta Taomac kutokana na kile ilichodai ni kukiuka sheria za biashara ya ushindani baada ya kukaa na kujadiliana kuhusu mgomo.

Wiki iliyopita, Bisarara alikaririwa na vyombo vya habari akisema kwamba kutokana na bei elekezi iliyotolewa na Ewura, wafanyabishara wanapata hasara ya Sh150 mpaka 250 kwa kila lita hivyo kampuni hizo zitaweza kutoa huduma hiyo chini ya mwezi mmoja tu.

Ewura yatoa tamko
Kwa upande wake, Ewura imesema kuanzia jana, kampuni 13 ziliuza petroli na dizeli kwa ajili ya kusambazwa kwenye vituo vya rejareja.Taarifa ya Ewura imesema mbali ya BP, Kampuni ya Camel Oil ilitoa petroli lita 416,500 na dizeli 626,000, OilCom ilitoa petroli lita 353,000 na dizeli lita 382,000, Total ilitoa dizeli lita 163,000 na ORYX ilitoa petroli lita 44,000 na dizeli lita 91,000.

Kampuni ya Gulf Bulk ilitoa petroli lita 86,500 na dizeli 272,000, Engen ilitoa lita 64,000 za petroli na lita 175,000 za dizeli, MGS International ilitoa lita 116,000 za petroli.

Nat Oil ilitoa petroli lita 55,000 na dizeli 79,000. Lake Oil ilitoa lita 65,000 za petroli na dizeli lita 279,500. Gapco ilitoa petroli lita 418,100 na dizeli lita 348,500.

Kampuni ya Hass ilitoa petroli lita 119,000 na dizeli lita 57,500 wakati Kobil ilitoa lita za petroli 37,000 na lita 431,000 za dizeli.
 
(Habari hii ni kwa mujibu wa mtandao wa gazeti maarufu la Mwananchi)

 

Samsasali blogspot. Huyu jamaa ni noumer!

Kibogoyo Wake Mtori, Supu ataambulia Mchuzi.

Ni matumaini yangu ya kuwa wote tu wazima baada ya Long Weekend leo wengi tumerejea katika shughuli zetu za kile siku. Poleni na pilika pilika za Mafuta hapa mjini Dar-es-Salaam hali imekuwa tata, leo nimesikia watu wakiwalaumu EWURA kusababisha matatizo kwani wao walikuwa wananunua bei hiyo wanayotaka kimbelembele cha EWURA kujifanya inawajali wananchi kumbe ndo imewakera wananchi hahaha Tanzania ni Zaidi ya uijuavyo.

Ninakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya Friends On Friday ya tarehe 5 August, 2011 haikuwa ya Kitoto Sifa na Utukufu tunamrudishia Mungu.

Katika utafiti wangu nimegundua watu wengi sana maarufu ama mashuhuri, umaarufu wao na umashuhuri wao uliwajia kama ajali, haikuwa katika moja wapo ya plan za maisha kufika pale walipofika, ndio maana wengi wao huwa hawadumu katika kile kilichowaweka juu, utakuta mtu ame struggle kufika sehemu fulani katika maisha ila akifika hapo juu anaanza kufanya mambo yanayommaliza yeye mwenyewe.

Shauku yangu nikiona watanzania hasa vijana kila Mtu aki simama kutimiza ndoto ya maisha yake, na nini unafanya kutimiza ndoto za wengine pia, mimi kama leo nimenyanyuliwa ninafanyaje kuwainua wengine. Wabongo wengi sisi ni vibogoyo inapofika swala la kutimiza ndoto zetu. Wengi tunapenda mambo mepesi mepesi hatupendi Big Stuff.

Kuna msemo ambao ni maarifu sana ulioongelewa naAliyekuwa Kiongozi wa Marekani Aleanor Roosevelt, aliwahi sema "Great Mind discuss about Ideas, Average Minds discuss Events and Small Minds Discuss People"

(Mengi zaidi yapo katika blogu yake... Jamaa ni creative nimependa sana.. We kamcheki halafu urudi uniambie umeonaje?)